Social Icons

Pages

Friday, January 22, 2010




Mambo dada sijui nimekufananisha.


Nadhani unamjua kijana anaitwa..

Yule mvulana ni wangu tena ni mali yangu. (1)


Nani anajua majina wavulana wako wengi,

Ila kama unamzungumzia yule kijana basi umepotea.


Kwangu amefika na wala sijui kama anamwingine. (2)


Tusijegombana bure na urafiki ukatuisha.


Tangulini awe wako mwenyewe aishia kwangu



Kijana mahibibi tena mali yangu (1)


Sumu siniwekee ukamchukua aliye wangu


tusijegombana bure na urafiki ukatuisha


Vitu vyote vya thamani kwangu huniletea


Wala sijaomba, mwenyewe huja kujitetea


Sehemu mbalimbali tutakuja tembea (2)


Tusijegombana bure na urafiki ukatuisha


Siwezi amini uloyatamka mdomoni


nilidhani mimi nawe kama samaki na maji (1)


iweje leo utembee na wako shemeji


tusije gombana bure urafiki ukatuisha


Aliponiita baby hakusema tuko wengi


Mimi sikujua kama ana mwingine pembeni (2)


Mimi sina kosa dada naziomba samahani


Tusijegombana na urafiki ukatuisha.




Tusigombana bure na urafiki ukatuisha.

No comments: